Manara ametoa kauli hiyo kupitia ukurasa wake wa kijamii mara baada ya uongozi wa Simba kiujumla kuhudhuria shughuli za Bunge kwa siku ya leo kutokana na mualiko waliopewa na Spika wa Bunge Job Ndugai katika siku za hivi karibuni.
"Mabingwa wa nchi ndani ya mjengo, asanteni Wabunge wote kwa heshima kubwa mliyotupa leo. Nawaahidi mwakani kwa tutakayoyafanya mtatengua kanuni ili tuingie ndani na kuwa sehemu ya Bunge", amesema Manara.
Simba sasa imefikisha alama 68 kileleni katika michezo 28 ikiwa imebakiza mechi mbili kuweza kumaliza msimu huu.
