Spika Ndugai amtaka Bashe kuachana na umaarufu wa Mitandaoni

Spika wa Bunge, Job Ndugai amewatahadharisha wabunge wanaokusudia kupeleka hoja binafsi kuacha kutafuta umaarufu mitandaoni badala yake wafuate kanuni za bunge.

Ndugai ameyasema hayo leo Aprili 12 na kumtaja mbunge wa Nzega mjini, Hussein Bashe kuwa ni mfano wa wabunge hao ambao hutoa taarifa ya kusudio la kupeleka hoja binafsi lakini ghafla wanaanza kutangaza hoja zao mitandaoni.

"Wabunge wengine nawashauri mfuate kanuni na mfano ni Bashe, mnataka umaarufu tu wakati mnatakiwa kufanya lobbying (ushawishi) kwanza ili hoja zenu ziungwe mkono." amesema Ndugai.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo