Mahakama yatoa hukumu kesi aliyoingilia kati Rais

Mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza imetoa hukumu ya kesi iliyokuwa ikimkabili Afisa Mtendaji wa kata ya Mkuyuni jijini humo James Chorangirwe, aliyekuwa akituhumiwa kwa kosa la ubakaji na ulawiti, kesi ambayo Rais Magufuli aliingilia kati

Hukumu hiyo imetolewa na hakimu mkazi mfawidhi mwandamizi wa mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza Wilbert Chuma, baada ya kuridhika na ushahidi wa upande wa mashtaka, ambao ulidai kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo kati ya Novemba 14 hadi 16, 2016, na kumtaka kwenda jela miaka 30 na kulipa faini ya shilingi laki 8.
Mara ya kwanza shauri hilo lilifunguliwa mahakamani mwaka 2016 katika Mahakama ya Wilaya ya Nyamagana ambapo hakimu aliyekuwa anasikiliza alijitoa, baada ya kuwepo madai ya kupanga njama za kuharibu kesi, na mnamo Januari 2018, Rais John Magufuli aliingilia kati kwa kumuagiza mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella kufuatilia kwa karibu upelelezi, uendeshaji na hatima ya shauri hilo ili haki iweze kutendeka. 
Baada ya hapo Mkuu wa mkoa aliingilia kati na kuanza upya uchunguzi, na ndipo ilipothibitika muhumiwa huyo alitenda kosa hilo, na ndipo mahakama kutoa hukumu yake April 5, 2018.
Afisa Mtendaji huyo alishtakiwa kwa kosa la kubaka na kulawiti mwanafunzi wa darasa la tatu mwenye umri wa miaka 12.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo