Makete: Wananchi waikataa Taarifa ya Mapato na Matumizi


 Mwananchi Tito akichangia hoja kwenye mkutano huo
 Diwani wa kata ya Matamba Mh. Epheli Ng'ondya akifafanua jambo
Afisa mtendaji wa kata ya Matamba akisoma taarifa hiyo

Wananchi wa kijiji cha Matamba kata ya Matamba wilayani makete mkoani Njombe wamekataa kuipokea taarifa ya mapato na matumizi ya ujenzi wa daharia katika shule ya sekondari Matamba iliyopo kijijini hapo

Hayo yameibuka katika mkutano wa diwani wa kata hiyo na wananchi wa kijiji hicho, ambapo wananchi wamehitaji risiti zinazoonesha matumizi ya fedha hizo pamoja na mchanganuo wa kila kijiji kimechanga vipi

Afisa mtendaji wa kata hiyo ndiye aliyesoma taarifa hiyo ya mapato na matumizi kwa wananchi hao

Hali hiyo ikawafanya wananchi wahoji baadhi ya mambo waliyoona hayakwenda sawa katika taarifa hiyo lakini wakakubaliana kuwa ujenzi wa daharia hiyo utaendelea na watashiriki lakini taarifa hiyo ije kusomwa tena upya
  
Diwani wa kata hiyo Mh Epheli Ng'ondya akaungana na wananchi wake kuagiza maamuzi ya wananchi yafanyiwe kazi, lakini amewaomba wananchi kuendelea na ujenzi wa daharia hiyo hata kama wameikataa taarifa hiyo

Wananchi hao wakakubali kuendelea na ujenzi wa daharia hiyo huku diwani huyo akiwaasa wananchi kuwaepuka viongozi wa kisiasa wanaofika kwenye kata yake na kupiga siasa badala ya kufanya kazi kwani muda wa siasa haupo na kwa sasa ni wakati wa maendeleo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo