Mwalimu Ikonda: Inafika Hatua mwalimu unalazimika Kumchangia Mwanafunzi Chakula

Kutokana na umuhimu wa mwanafunzi kupata chakula shuleni, wakati mwingine huwalazimu walimu kutoa gharama zao wenyewe kuwanunulia chakula wanafunzi ambao wazazi wao hawajachanga fedha ya chakula

Hayo yamesemwa na Mwalimu mkuu wa shule ya Msingi Ikonda Enerika Kayombo na kusema yeye ni mmojawapo wa mwalimu ambaye amekuwa akitoa gharama zake kuhakikisha wanafunzi ambao hawajachangiwa chakula na wazazi wanapata chakula

"wakati wenzao waliochanga wanakula chakula, ambao hawajachanga unakuta wanakuwepo eneo wanapopata chakula wenzao, unawafukuza lakini wakati mwingine inakulazimu kugharamia ili wale, binafsi nimefanya hivyo, kamati ya shule ni mashahidi" amesema mwalimu huyo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo