Kesi hiyo ya jinai namba 296 ya Mwaka 2017 inaendeshwa na Hakimu Mkazi Ivan Msacky, ambapo washtakiwa wote 56 wanakabiliwa na mashtaka nane kila mmoja likiwemo la kufanya fujo kwenye uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Sofi wilayani Malinyi na kusababisha uharibifu wa mali ikiwemo kuchoma moto ofisi za serikali ya Kijiji.
Hakimu Msacky amesema, upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na pande zote mbili zimekubaliana kuanza kusikilizwa kwa kesi hiyo ifikapo Machi 28 mwaka huu,
Katika kesi hiyo upande wa Jamhuri unawakilishwa na Wakili Sunday Hyera akishirikiana na Edgar Bantulaki, ambapo upande wa utetezi unaongozwa na Barthlomew Tarimo, akishirikiana na Wakili Peter Kibatala.
