Mbunge awataja majeruhi ajali ya bomba la gesi

Mbunge wa Jimbo la Segerea kupitia CCM Bonnah Kaluwa, amethibitisha kuwepo kwa majeruhi wa ajali ya moto iliyotokea jana baada ya bomba la gesi kulipuka, katika eneo la Buguruni kwa Mnyamani

Kaluwa amesema majeruhi wapo watatu na wanaendelea na matibabu, lakini mmoja amekimbizwa kwenye hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi kutokana na kuwa na majeraha makubwa.

"Majeruhi wapo watatu, mmoja mwanamke moja mwanaume, yaani ule moto ulivyolipuka pale pembeni kuna wafanyabishara wanafanya biashara zao, kwa hiyo moto ulivyolipuka umempata mama mmoja kwenye mkono na shingoni, na baba mmoja ameungua kwenye mkono, na mtoto mmoja ambaye amepelekwa Muhimbili ambaye sijaweza kumuona, ameungua kichwanimni hao watatu", amesema Bonna Kaluwa.
Hapo jana kumetokea mlipuko wa moto baada ya bomba kubwa la gesi kupasuka kwa bahati mbaaya baada ya kugongwa na mafundi wa Dawasco, lakini mpaka asubuhi ya leo Jeshi la Polisi lilitoa taarifa kuwa hakukuwa na taarifa ya madhara kwa binadamu ikiwemo vifo au majeruhi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo