Ajiua baada ya kukosea kutuma meseji

Binti mmoja nchini Uingereza mwenye umri wa miaka 17, Charlotte Guy, amejiua kujiua baada ya kukosea kutuma meseji na kwenda kwa mpenzi wake badala ya rafiki yake

Charlote ambaye alikuwa akimtumia rafiki yake meseji kwa kutumia snapchat akimwambia kuwa amelala na mwanaume mwengine, alikosea kutuma meseji hiyo na kwenda kwa mpenzi wake Jack Hurst  mwenye umri wa miaka 20.
Watu wa karibu wa wawili hao wamesema kwamba baada ya kufanya hivyo alimtumia meseji ya kumuomba radhi Jack na kumuaga ikisema ..”Kwa heri, tafadhali nisamehe, nakupenda, lakini kujua kuwa unanichukia inatosha”.
Baada ya hapo Jack alianza kumtafuta kwenye simu mpenzi wake huyo bila mafanikio na kuamua kuita polisi na kwenda chuoni kwao kumtafuta, na kukuta amejinyonga karibu na eneo la chuo alichokuwa akisomea masuala ya afya.
Jack Hurst ambaye ni mpenzi wa Charlote


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo