Makamu wa Rais Mama Samia alivyohamia Rasmi Dodoma leo

Makamu wa Rais, Samia Suluhu leo Ijumaa Desemba 15 amehamia rasmi makao makuu ya nchi  ikiwa ni mwendelezo wa Serikali ya Awamu ya Tano kuhamia Dodoma.

Akizungumza mara baada ya kuwasili nyumbani kwake Kilimani mjini Dodoma, Samia ameomba wananchi wa mkoa huo kuonyesha ushirikiano katika kufanya kazi ili kulisukuma gurudumu la maendeleo

"Nilikuwa hapa kwa muda mrefu kidogo lakini nilipangiwa kuhamia rasmi leo Desemba 15 na nimefurahi kwamba nitafanya kazi mahala pangu pa kazi pa kudumu," amesema Samia.

Amesema kauli mbiu yake kwa wakazi wa Dodoma ni kuufanya mji huo kuwa wa kijani hivyo Desemba 21 ataendesha mpango wa kupanda miti katika wilaya zote.

"Kwa kuwa nasimamia pia masuala ya mazingira nitaendesha zoezi hilo ili kurudisha hali ya Dodoma," ameongeza.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo