Wananchi wa Shehiya ya Kiomba mvua Wilaya ya kaskazini B wahofia maisha yao kutokana na uwepo wa baa ya mabatini inachangia kuongezeka vitendo viovu ikiwemo vya wizi na ubakaji katika maeneo yao.
Wakizungumza nje ya Mahakama ya Wilaya ya Mfenesini Katibu wa Sheha Shehia hiyo Semeni Juma Nyange na baadhi ya wananchi wamesema hali ya usalama wao umekuwa hatarini tokea kuwepo kwa baa hiyo kwani vijana wengi wanao jihusisha na ulevi hutumia shehia hiyo kufanyia mambo yao maovu ikiwemo wizi,uhalifu wa aina mbalimbali.
Wamesema wamekuwa wanashindwa kufanya shughuli zao za kijamii kutokana walevi wakisha lewa hujifisha kwenye mapori na kutishia kuwabaka wanawake na watoto wanao kwenda kutafuta kuni.
Wakizungumzia hatua walizozichukua ili baa hiyo iondoshwe wamesema malalamiko yao waliyafikisha katika ngazi mbalimbali ikiwemo ngazi ya shehia,Wilaya hadi Mkoa lakini bado halijafanyiwa ufumbuzi hivyo wameiomba mahakama ya vileo kutowapa kikali wamiliki wa baa hivyo kwa mwaka 2018 ili kunusuru vizazi vyao.
