Malalamiko ya wananchi yatasaidia wamiliki wa Baa kunyimwa vibali

Jumla ya baa kumi na nne za Wilaya ya Mjini   leo zimefika katika mahakama ya Vileo Zanzibar Mwanakwerekwe  kwa ajili ya kuomba  kibali  cha  kuendeshea  biashara  ya Vileo   kwa mwaka 2018.
Akizungumza nasi Mwenyekiti wa Mahakama ya Vileo Zanzibar Mohammed Subeit amesema amepokea maombi kumi na nne  ya wamiliki wa mabaa  kwa ajili ya kuendesha shughuli za vileo  katika maeneo yao ya biashara.
Aidha amesema  ni muda muwafaka  sasa kwa wananchi wa Wilaya ya mjini kufika mahakamani  kwa ajili ya upingaji  wa maombi hao  kama kuna baa   zinazoleta usumbufu  kwao ikiwemo   kupiga miziki kwa sauti kubwa,zilizopo katika  makaadhi ya wananchi,na zile  zisizofata  sheria kwa wananchi.
Hata hivyo Subeit amesema endapo  hakutakuwa na  wapingaji  kwa baa hizo  na mahakama ikajiridhisha   kisheria  basi hakutakuwa na sababu  kwa   baa hizo kunyimwa kibali kwa ajili ya kuendesha biashara  ya vileo.
Na:Amina Omar. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo