Katibu wa CWT afariki Dunia

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Yahya Msulwa amefariki dunia jana katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.
Katibu mkuu wa zamani wa chama hicho, Gratian Mkoba ameithibitisha Mwananchi leo Ijumaa Novemba 17 wakati akizungumza kwa simu.
Mkoba amesema, “Ni kweli amefariki jana usiku na alipelekwa jana hiyo usiku kwa mujibu wa ndugu zake walionipa taarifa, maana mimi nilikuwa nina wiki moja hatujawasiliana na sijui alikuwa na anasumbuliwa na nini,”amesema Mkoba.
Amesema hivi sasa yupo njiani kwenda nyumbani kwa marehemu Tuangoma kujua taratibu za mazishi.
Chanzo: Mwananchi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo