Chaula: Pamoja na Figisu Nilizofanyiwa Sitoki CCM Ng'o

Aliyekuwa mwenyekiti wa CCM wilaya ya Makete Francis Chaula amesema licha ya jina lake kuenguliwa katika kugombea uenyekiti wa chama hicho, hana mpango wa kukihama chama cha Mapinduzi

Ndugu Chaula ameyasema hayo wakati akihutubia mkutano wa chama hicho muda mchache kabla ya kujiuzulu nafasi hiyo kupisha uchaguzi ufanyike wa kumpata mwenyekiti mpya, ambapo amesema pamoja na figisu alizofanyiwa na baadhi ya watu lakini "hatoki mtu hapa" akimaanisha hatakihama chama cha Mapinduzi

"Naombeni mseme kama nayosema mimi, nikisema hatoki mtu hapa na nyie muitikie hivyo hivyo, maana kuna watu wanafikiri wakinifanyia figisu ndio nitaondoka CCM sasa nawaambia hivi, haondoki mtu hapa" amesema Chaula

Alitumia muda huo pia kuelezea aliyoyafanya ndani ya chama tangu aingie madarakani 2012 kuwa ni pamoja na kufanikisha ujenzi wa ofisi mpya za CCM wilaya ambazo zimeanza kutumika, kutembelea kata zote za wilaya ya Makete kusikiliza kero za wanachama, kutumia fedha zake binafsi kufanikisha shughuli za chama

Jana Novemba 25, Onna Nkwama alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa 4 wa chama hicho wilaya akimrithi Francis Chaula aliyemaliza muda wake

Tangu wilaya ya Makete kuanzishwa chama cha mapinduzi kimeongozwa na wenyeviti wanne ambao ni Amosi Sukunala Nkwama, Jasel Mwamwala, Francisa Chaula na sasa ni Onna Nkwama


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo