Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustino Olomi amesema watu hao walizama jana Jumatatu saa 6:30 mchana, ambapo mwili Adela Andrea (26), mkazi wa Kijiji cha Itongo umeopolewa na Nelson Boniphace (20), mkazi wa Kisiwa cha Ilamba aliogelea na kuokolewa.
Kamanda Olomi amesema, miili ambayo haijapatikana ni ya Superius Severine (27) mkazi wa Kijiji cha Nyakitaba na Evelius Zephrine (22) mkazi wa Mubunda Kitoko wilayani Muleba
Olomi amesema mtumbwi huo uliokuwa na madumu 33 ya maji amesema unamilikiwa na Rashidi Sabini (33), mkazi wa Kijiji cha Ilamba na kwamba ulizama baada ya kupigwa na mawimbi kutokana na upepo mkali
