Wafanyabiashara Makete waagizwa Kutunza Kumbukumbu ili wasikwepe Kodi

Rai imetolewa kwa wafanyabiashara wilayani Makete mkoani Njombe kutunza kumbukumbu za biashara zikiwemo za manunuzi ili kutoleta mkanganyiko wa kiasi cha kodi anachostahili kulipa mfanyabiara wakati wa ulipaji wa kodi

Akitoa elimu kwa mlipa kodi kwa wananchi wa Tandala na maeneo ya jirani katika semina iliyofanyika katika ukumbi wa MTC Tandala  yenye lengo la kuongeza mapato ya serikali na kupitia mabadiliko ya sheria ya kodi kwenye bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2017/2018, afisa elimu na huduma  kwa mlipa kodi kutoka mamlaka ya mapato Tanzania TRA Kefa Mwambene amesema ni vema wafanyabiashara wakatunza kumbukumbu za biashara zao ili kutoleta mikanganyiko baina ya maafisa wa TRA na wafanyabiashara wakati wa ulipaji kodi

Awali wafanyabiashara walipata nafasi ya kuuliza maswali na kutoa mapendekezo ya namna bora ya ukusanyaji wa mapato na kujenga uhusiano baina ya TRA na wateja wake huku wakieleza adha wanayoipata wakati wa operesheni mbalimbali zinazofanywa na mamlaka hiyo kupitia wakala wake kampuni ya YONNO ACTION MART na baadaye  afisa  wa TRA akatolea ufafanuzi

Green fm imefanya mahojiano na wafanyabiashara Nje ya ukumbi mara baada ya kumalizika kwa semina hiyo na kuelezea jinsi semina hiyo ilivyowasaidia kutambua mambo mbalimbali  ikiwemo majukumu na haki ya mlipa kodi

Katika mwaka wa fedha 2017/2018 serikali imepanga kukusanya kiasi cha shilingi trilioni 31.7  kupitia vyanzo vya mapato mbalimbali ambapo mamlaka hiyo ya  mapato Tanzania pekee imepanga kukusanya shilingi trilioni 17 katika bajeti hiyo


Na Riziki Manfred


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo