FULL AUDIO: Walimu wa Makete Njombe wafunguka Mazito

Mwalimu Gregory Emmanuel
Image result for cwt wilaya ya Makete
Mwalimu Thobis Kasambala

Wakati Oktoba 5 ya kila mwaka Dunia huadhimisha siku ya walimu, baadhi ya walimu wilayani Makete mkoani Njombe wameonesha kufurahia wao kuwa walimu huku wengine wakiiomba serikali kuwalipa madai yao

Wakizungumza na Green FM walimu hao Wakiwemo Tobisa Kasambala, Gregory Emannuel na Mchungaji Luka Lwila wamesema walimu ni nguzo muhimu katika jamii ambayo imesaidia kuielimisha jamii kwa kuwa kila mtu kwa nafasi yake amepitia mikononi mwa walimu bila kujali ni mwalimu wa mfumo rasmi ama asiye wa mfumo rasmi

Miongoni mwa walimu hao Bw. Thobias Kasambala amesema anaipongeza serikali ya awamu ya 5 katika kutekeleza baadhi ya mambo ikiwemo kuondoa watumishi hewa ambapo na walimu wameguswa na wao kama walimu wanaunga mkono uamuzi huo wa serikali

Siku ya walimu duniani  imekuwa ikiadhimishwa kila mwaka ifikapo oktoba 5 na mtandao wa elimu  Tanzania TENMET, lakini hapa nchini imekuwa ikiadhimishwa kila baada ya miaka 3, Na hatua hiyo imekuja baada ya makubaliano yaliyofanyika mjini paris mwaka 1966 baina ya shirika la  elimu na utamaduni  duniani UNESCO na shirika la kazi duniani ILO.

Sikiliza sauti zao kwa kubonyeza Play hapo chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo