BARABARA NYINGINE YAFUNGWA NA KUSABABISHA USUMBUFU MKUBWA

lori lenye namba T 410 AFR likiwa limeharibika sehemu yenye kona kitu kinachofanya magari makubwa yasiweze kabisa kupita eneo la Ilamba wilaya ya kilolo mkoani Iringa
  • Na Denis mlowe - aliyekuwa Kilolo
  • Magari yote ya abiria yanayofanya safari zake za kwenda kati ya Iringa mjini na Kidabaga wilaya ya Kilolo  yamekwama kwa wiki baada ya loli lilobeba magogo kuziba njia maeneo ya Ilamba na kufanya kutokuwa na mawasiliano kati ya kidabaga  na Iringa mjini.

    Tukio  hilo  limetokea wiki sasa kwa mujibu wa madereva wa mabasi yanayofanya safari zake kati ya Iringa mjini na Bomalang'ombe na kufanya magari madogo kupita kwa tabu eneo liliharibika lori hilo lenye namba T 410 AFR kwa upande cabin yake na tela lenye namba T 471 ATY mwenye mali hajajulikana na kusababisha msafara wa mbunge wa viti maalum kuchukua nusu saa kuweza kuvuka eneo hilo kutokana na ubovu wa nafasi lilipoharibika.

  • Baadhi ya abiria  na mashuhuda wa  tukio  hilo waliozungumza na mtandao huu  eneo la  tukio  wamedai kuwa lori hilo lilianza kuziba njia kila linapoharibika kitu kinachofanya magari makubwa yasifanye biashara ya kusafirisha abiria kutokana na ufinyu wa barabara hiyo
    .


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo