Rais Magufuli: Tulikuwa Tunaenda Kuzimu

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli amesema kutokana na matendo maovu yaliyokuwa yanaendelea serikalini, nchi ilikuwa inaelekea kuzimu

Rais Magufuli ameyasema hayo leo wakati akifungua mkutano wa 33 wa jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania jijini Dar Es Salaam ambapo amesema miongoni mwa vitu vilivyokuwa vinafilisi nchi ni watumishi hewa na wenye vyeti hewa

Rais amesema "Kwa sasa kero hiyo imeondoka baada ya kudhibiti na kuwaondoa watumishi hewa na wale waliokuwa na vyeti hewa, unakuta mtu ni kilaza hajasomea anachokifanyia kazi, wewe uliyesomea mnajikuta mnalipwa mshahara mmoja, hii ilikuwa inaumiza sana, lakini sasa nidhamu imerejea"


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo