CCM: Jimbo la Monduli Tutalikomboa Lirudi CCM

WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Monduli mkoani Arusha wamedhamiria kwa pamoja kulikomboa Jimbo la Monduli pamoja na kupata viongozi wengine wanaotokana na chama hicho ili kupata maendeleo.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya hiyo, Loota Sanare wakati wa uchaguzi wa viongozi wa CCM Wilaya uliofanyika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Monduli. Wanachama hao kwa kauli moja walisema wamedhamiria kulikomboa jimbo hilo ambalo kwa sasa linaongozwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).


Sanare alisema hakuna asiyejua kuwa Wilaya ya Monduli inaangaliwa kwa jicho la kipekee kwa sababu ya mambo mbalimbali ya kisiasa ikiwemo ya vyama na makundi, lakini baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kuhamia Chadema kugombea Urais, baadhi ya wanachama walihama naye na kusababisha misukosuko ndani ya CCM.

Alisema lakini kwa kuwa CCM ipo imara, wamejipanga kuondoa mamluki ndani ya chama hicho kwa kuchagua viongozi bora watakaowezesha jimbo hilo kurudi CCM. “Lowassa aliletea misukosuko kabla ya kuhama chama kwa sababu alikuwa akitaka wagombea fulani ndiyo wawe viongozi, lakini hivi sasa hakuna hilo hatutaki mamluki ndani ya chama chetu ndiyo maana amehama na 2020 tutalichukua jimbo hili ,” alieleza Sanare.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo