Bibi Akutwa akiwa amefia Mtoni wilayani Makete

Mwanamke mmoja Christina Mbilinyi anayekadiriwa kuwa na umri wa zaidi ya miaka 70 mkazi wa kijiji cha Lupalilo wilayani Makete mkoani Njombe amekutwa akiwa amekufa katika mto kijijini hapo

Tukio hilo la kupatikana akiwa amefariki dunia limegundulika leo baada ya taarifa za kupotea kwake kutolewa kijijini hapo tangu jumamosi, lakini leo wanakijiji wakaamua kuendesha msako wa kuanza kumtafuta katika maeneo aliyopita wakati anaondoka

Akizungumza na mwandishi wetu ndugu wa karibu wa Marehemu alikokuwa akiishi kijijini hapo amesema Ijumaa ya Septemba 29 mwaka huu Marehemu aliaga kuwa anakwenda kusalimia ndugu zake waliopo katika kijiji cha Usagatikwa na alifika kwa ndugu zake hao

Amesema Septemba 30 marehemu huyo aliondoka kwa ndugu zake wa Usagatikwa kurudi nyumbani anakoishi Lupalilo lakini hakufika nyumbani kama ilivyotarajiwa hali iliyowapa mashaka na kuanza kumtafuta kabla ya kukutwa akiwa amefariki katika mto huo

Diwani wa kata ya Lupalilo Mh Imani Mahenge naye amezungumzia tukio hilo kwa kusema baada ya kumpata mkazi huyo akiwa amefariki alitoa taarifa kwa jeshi la polisi

Jeshi la polisi wilaya ya Makete limefika eneo la tukio kwa ajili ya kukamilisha taratibu zao kwa mujibu wa sheria, ambapo baada ya uchunguzi ndugu wamekabidhiwa mwili wa marehemu kwa ajili ya maziko










JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo