Waziri ampa wiki moja mtendaji

Naibu Waziri wa Tamisemi Seleman Jafo ametoa wiki moja kwa mtendaji mkuu wa Shirika la Elimu Kibaha kuanza mara moja upanuzi wa majengo baada ya kubaini kuwa maradi huo umekwama kwa kipindi cha miaka saba

Naibu Waziri amefikia uamuzi huo baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali teule ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani, Tumbi Septemba 27 mwaka huu na kubaini kusimama kwa mradi huo kwa muda mrefu.
Akizungumza na watumishi wa Hospitali hiyo pamoja na viongozi wa Mkoa Naibu Waziri Jafo ameeleza kusikitishwa na namna ambavyo mradi huo umetelekezwa kwa miaka saba hali ambayo imesababisha majengo kuchakaa kabla hata ya kuanza kutumika.
“Natoa wiki moja kwa Mtendaji mkuu kufanya haraka iwezekanavyo ujenzi wa mradi huu wa upanuzi ambao ulikuwa umesimama kwa kipindi kirefu uanze mara moja maana fedha zipo na tumeshazitoa shilingi milioni 600 sasa sijui nini tatizo kwa hiyo wiki ijayo nataka kuona ujenzi huo unaanza kuendelea”, amesema Jafo.
Aidha Waziri Jafo alipata fursa ya kusalimiana na wagonjwa waliolazwa Hospitalini hapo kwaajili ya kupata huduma za afya.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo