TFF Yaikoa Yanga "Isizamie" Algeria

Wachezaji wa Yanga wanatarajia kuondoka leo usiku nchini Algeria kurejea nyumbani.

Sasa wanatarajia kuondoka na ndege ya Emirates badala ya Turkish Airways na imeelezwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limelazimika kutoa mkopo kwa klabu hiyo ili kuwakomboa.

Wachezaji saba na Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa walichelewa ndege jijini Algeria na kulazimika kusubiri hadi Jumanne kesho ndiyo waondoke na kutua nchini kesho.

Mkwasa alisema wataomba msaada kwa MC Alger waliokwenda kucheza nao na kufungwa mabao 4-0 kwa kuwa hawakuwa na fedha za kutosha.


Lakini msaada huo wa TFF utawafanya warejee haraka nyumbani na si Jumatano tena kama ambavyo ilikuwa ikitarajiwa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo