Mume ajiua Baada ya Kukutwa na VVU, Mkewe akutwa Hana

NA SALVATORY KUTOKA KAHAMA

Katika hali isiyokuwa ya Kawaida Mkazi wa Mtaa wa Shunu mjini Kahama, FIKIRI DAUDI (38) amejinyonga kwa kamba ya katani usiku wa kuamkia leo baada ya kupimwa na kubainika kuishi  na virusi vya Ukimwi (VVU).

Mjane wa FIKIRI, SHIJA JULIUS amesema baada ya kupima afya zao Mume wake alibainika kuwa na maambukizi ya VVU huku yeye akiwa hana virusi hivyo jambo ambalo lilimkera na kuamua kuchuka uamuzi huo.

Miongoni mwa mashuhuda wa tukio hilo, SENIFROSA DAUDI amesema taarifa za kujinyonga kwa FIKIRI zimezua majonzi miongoni mwa wakazi wa mtaa huo.

Naye mwenyekiti wa mtaa huo, KUBE SHIJA amewataka wananchi wa mtaa huo kuacha kuwanyanyapaa watu wenye VVU ambapo amesema kwa mujibu wa majirani Mke wa Marehemu FIKIRI alianza kumnyanyapaa Mume wake hali iliyosababisha achukue uamuzi huo wa kujinyonga.

SHIJA amesema mwili wa Marehemu umechukuliwa na Jeshi la Polisi na kupelekwa katika hospitali ya Halmashauri ya  Mji wa kahama kwaajili ya Uchunguzi na baada ya hapo watakabidhiwa ndugu kwaajili ya taratibu za mazishi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo