Wakulima Rungwe waidai serikali hati ardhi

Na Kenneth Ngelesi, Rungwe

Umoja wa Wakulima Wadogowadogo Nyanda za juu kusini tawi la  Rungwe (RUMBIAA)wameiomba serikali kuharakisha mpango wa kutoa hati za kimila za kumiliki ardhi kwa wakulima hao.

Aidha Chama hicho kimeitaka serikali kuangalia namna ambavyo fursa zinazopatikana katika mipango yake husuasani katika suala la kilmo kwanza  zinawafikia na kuwanufaisha wakulima hao kupitia chama chao

Akizungumza na mtandao huu wilayani hapa Mratibu wa Chama hicho Brown Mwangate mara baada ya kikao  cha kawaida ngazi ya Wilaya ambapo mambo mbalimbali yalijadiliwa likiwemo suala la wakulima kukosa hati miliki za kimili za umiliki ardhi.

Mwangate alisema kuwa  serikali imekuwa ikitoa matamko mara kwa mara juu ya kutoa hati hizo kwa wakulima lakini suala hilo limekuwa likienda kwa kasi ndogo hali inayowafanya  washindwe kunufaika na ardhi zao.

Alisema kutokana na Wilaya hiyo kuwa na uzalishaji mkubwa  wa mazao ya ndizi pamoja na viazi na matunda  hivyo kitendo cha wao kupatiwa hati hizo kutasaidia kuongeza tija ya uzalishaji ya mazao mengine hasa  kilimo cha kahawa.

Aidha katika hatua nyingine wakulima hao wameomba serikali kuwasaidia namna ya kupata wawekezaji  watakao jenga viwanda vya usindikaji wa matunda hasa ndizi na mtunda  kwani kuna uwezekano mkubwa wa kupata malighafi hasa juice na  biskuti  hali ambayo itapunguza gharama za uagizwaji  bidhaa hizo nje ya nchi.

Mratibu huyo alisema suala jingine litakalo saidia katika hatua ya upatikanaji wa wawekezaji ni kupunguza tatizo la ajira  na kuongeza hali ya upatikanaji wa masoko kiurahisi zaidi.

Pia mratibu huyo amesema lengo la kuanzisha chama  hicho ni  kumuwezesha mkulima kufikia mafanikio bora kupitia kilimo kwa kushirikiana  na serikali na Taasisi binafsi mabenki na jamii kwa ujumla.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo