Mahindi ya Ghala la Serikali Yakutwa Yameharibiwa na Wadudu

Wakati wananchi katika halmashauri za wilaya zaidi ya 55 nchini wakikabiliwa na uhaba Mkubwa wa chakula imebainika huwenda zaidi ya tani 86,222 za mahindi yaliyohifadhiwa kwenye ghala la chakula kituo cha Shinyanga zipo katika hatari ya kuharibiwa na wadudu waharibifu

hali hiyo imeonekana baada ya kamati ya kudumu ya bunge ya kilimo mifugo na maji kutembelea ghala hilo na kujionea jinsi mahindi yaliyohifadhiwa hapo yalivyoharibika huku yakiwa yanatoa wadudu

Baadhi ya wajumbe hao wameiomba serikali kuangalia upya suala la mahindi hayo yasiwe yanahifadhiwa muda mrefu wakati wananchi wakiwa wanalalamikia suala la njaa kutokana na mvua kunyesha na badala yake wauze mahindi hayo kwa bei nafuu

Pamoja na wajumbe wa kamati hiyo kujionea mahindi hayo yakiwa na wadudu aina ya funza Mtendaji mkuu wa maghala ya Chakula hapa nchini Deusdedit Mpazi amesema kuwa hali hiyo iliyopo haimaanishi kuwa mahindi hayafai kutumika

Naibu waziri wa kilimo mifugo na Uvuvi William Ole Nasha amekiri kuwa kuna baadhi ya wilaya ambazo wananchi wake wanakabiliwa na njaa na serikali inatambua suala la kuwapelekea chakula cha bei nafuu linafanyika


Kamati ya bunge ya Kilimo mifugo na Uvuvi ipo mkoani Shinyanga kwa ajili ya kukagua miradi ya maji na kujionea shughuli zinazofanywa kupitia fedha za serikali na taasisi zisizokuwa za serikali


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo