Young Dee azijibu tetesi za kurudia unga

Hatimaye rapper Young Dee amejibu kwa ufupi kuhusiana na tetesi kuwa amerudi tena kwenye matumizi ya dawa za kulevya.
Akiandika maneno mafupi sana kwenye post yake mpya ya Instagram, Young Dee amedai kuwa ‘muda utaongea.’
“Time will Tell… Mi sina tatizo na mtu… Tuombeane kheri tu… Siwezi shindana na maneno,” ameandika rapper huyo.
Wiki hii tetesi za kuwa Dee amerejea tena kwenye utumiaji wa dawa hizo zilianza kufuatia maneno ya meneja wake Max mtandaoni. Max alida kuwa rapper huyo ameanza tena kuubwia unga na kwamba amechoka kusumbuka naye.
Tetesi za Young Dee zimekuja katika kipindi ambacho watanzania wanasikitishwa na hali walizonazo Chidi Benz na Nando kutokana na kuathirika vibaya na madawa hayo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo