AUDIO: Vifijo Vyatawala Kiguru Makete, Ni Baada ya Gari Kufika Kwao Tangu Dunia Iumbwe

Muonekano wa daraja la barabara ya kwenda Kiguru kama ilivyopigwa na mtandao huu mwaka 2013
Serikali imepongezwa kwa kufanikisha uwepo wa barabara katika Kata ya Kiguru wilayani Makete mkoani Njombe ambapo kwa mara ya kwanza mwaka huu Gari limeweza kufika katika kata hiyo

Akizungumza na mwandishi wetu katika mahojiano maalum Diwani wa kata ya Kiguru Mh Simon Mwaikenda amesema wananchi wa kata hiyo wamekuwa wakipata tabu kufuata huduma mbalimbali hasa za matibabu kwa kuwabeba wagonjwa kwenye machela kwa umbali mrefu mpaka halmashauri ya Busokelo mkoani Mbeya kupata huduma za hospitali

Amesema wazo la kuanzisha barabara ya kwenda katika kata yake lilianza mwaka 1958 na mafanikio yameonekana mwaka huu wa 2017 ambapo barabara imekamilika na kupitika kwa gari mpaka kwenye kata hiyo

Kufuatia kukamilika kwa barabara hiyo ameelezea kutakuwa na manufaa na kufungua fursa za kiuchumi na maendeleo katika kata hiyo, pamoja na uharaka wa kuwapeleka wagonjwa ama kina mama wajawazito kupatiwa matibabu ya rufaa nje ya zahanati ya kijiji chao, ambapo ni hospitali zilizopo halmashauri ya Busokelo wilayani Rungwe mkoani Mbeya


Amesema wananchi walijawa na furaha kuona gari kwa mara ya kwanza limefika katika kata hiyo tangu ianzishwe, na kuipongeza serikali kwa jitihada hizo za kufanikisha utatuzi wa kero hiyo ya muda mrefu
Sikiliza sauti hapa chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo