![]() |
Kaimu Meenja Uhusiano TANESCO, Bi.Leila Muhaji |
NA K-VIS BLOG.
SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema, kwa sasa linafanya mabadiliko ya uongozi wa ndani ya Shirika kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za Shirika kwa lengo la kuongeza ufanisi zaidi na kazi hiyo ambayo tayari imeanza itakapokamilika, Umma wa Watanzania utahafahimshwa kupitia vyombo vya habari.
Taarifa fupi iliyotolewa na Ofisi ya Uhusiano Makao Makuu TANESCO leo Januari 5, 2017 imeviomba vyombo vya habari vitoe fursa fursa kwa Mamlaka husika kuendelea kukamilisha zoezi hili muhimu kwa maendeleo ya Shirika na Taifa kwa ujumla na taarifa rasmi itatolewa baada ya zoezi kukamilika.