Mvua yazua balaa Shinyanga,Nyumba zaidi ya 20 zaezuliwa

Nyumba zaidi ya 20 zimeezuliwa na upepo mkali wakati mvua ikinyesha usiku huu wa Januari 11,2017 katika manispaa ya Shinyanga.(Habari na RUVUMATV)

Hadi sasa bado haijafahamika kama kuna vifo ingawa mamlaka husika haijatoa taarifa kuhusu tukio hilo, mvua hiyo iliambatana na upepo mkali pia imejeruhi watu kadhaa katika kata ya Kitangiri manispaa ya Shinyanga.

Diwani wa kata ya Ngokolo kupitia chama cha Demoklasia na Maendeleo(CHADEMA) Emmanuel Ntobi akipewa maelezo na mmoja wa wahanga ambaye amejeruhiwa na paa la nyumba.

Diwani wa kata ya Ngokolo kupitia chama cha Demoklasia na Maendeleo(CHADEMA) Emmanuel Ntobi amefika katika baadhi ya maeneo yaliyoathiriwa na kujionea uharibifu uliojitokeza kufuatia mvua hiyo

Nyumba zaidi ya 20 pia madarasa manne na ofisi ya walimu katika shule ya msingi Viwandani zimeezuliwa. Amewaomba wasamaria wema kufika katika eneo hilo ili kutoa msaada kwa wananchi waliothirika na mvua hiyo.

Nyumba zilizoharibiwa na mvua .

Diwani wa kata ya Ngokolo kupitia chama cha Demoklasia na Maendeleo(CHADEMA) Emmanuel Ntobi akipewa maelezo na mmoja wa wahanga ambaye amejeruhiwa na paa la nyumba.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo