AUDIO:Tamko la Serikali Kuhusu Maafa yaliyoikumba Isapulano Makete

Mkuu wa Wilaya ya Makete Veronica Kessy
Image may contain: mountain, sky, outdoor and nature
HERI YA MWAKA MPYA!
Ndugu wananchi wa Makete na Watanzania wote kwa ujumla,wananchi wa kijiji cha Isapulano katika kata ya Isapulano hapa Wilayani Makete wamepatwa na maafa mnamo tarehe 02/01/2017

Maafa hayo yalisababishwa na mvua kubwa iliyoambatana na upepo,jumla ya nyumba 16 zenye jumla ya watu 37 ziliathirika kwa viwango tofauti


Katika tukio hilo waliumia watu wawili,wakapatiwa matibabu katika Zahanati ya Isapulano na kwa bahati nzuri wanaendelea vizuri,Aidha tunamshukuru Mungu hakuna mwananchi aliyefariki

Ndugu wananchi nyumba hizo zinahitaji vifaa vya ujenzi yaani matofali, saruji, mbao, misumari, mabati n.k, pia wananchi walioathirika wanahitaji kusaidiwa mahitaji ya kibinadamu kwa hiyo nawaomba wananchi na wadau wote wa ndani na nje ya Wilaya ya Makete tuguswe kwa namna moja ama nyingine kuchangia fedha au vitu ili kuwasaidia wananchi hao

Kwa sasa wananchi hao wamehifadhiwa na majirani na ndugu zao,Aidha wananchi wa kijiji hicho wameanza kujitolea kusaidia ujenzi huo

Ninawashukuru na kuwapongeza kwa jitihada hizo,nawasihi tuwaunge mkono kwa kutoa misaada ya hali na mali,michango ya fedha iingizwe kwenye Akaunti ifuatayo iliyopo NMB MAKETE

Jina la Akaunti:Kijiji cha Isapulano 
Namba ya Akaunti:60410004408


Na msaada wa vitu au vifaa uwasilishwe kwa Mtendaji wa kata ya Isapulano Bi.Tabu Mohamed mwenye namba 0745571046
Ahsanteni sana Ni mimi Veronica Kessy Mkuu wa Wilaya ya Makete

Chanzo:Kitulo FM Radio

Sikiliza sauti yake hapa chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo