AUDIO: Ujenzi wa Nyumba za NHC Makete Mjini, Naibu Waziri atoa ya Moyoni


Nyumba za NHC zilizojengwa Ngiu Makete

Msafara wa naibu waziri ukiwasili katika nyumba hizo
Naibu waziri wa ardhi Nyumba na maendeleo ya Makazi Mh Anjelina Mabula ameishauri jamii na wadau mbalimbali wa maendeleo kujitokeza kununua nyumba zinazojengwa na shirika la nyumba la taifa NHC zilizopo eneo la Ngiu Makete mjini wilayani hapo

Naibu waziri ameyasema hayo leo katika ziara yake ya kikazi aliyoifanya wilayani hapo ambapo mbali na kuzungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Tandala wilayani Makete, pia ametembelea ujenzi wa nyumba hizo zipatazo 30 ambao upo katika hatua za mwisho za umaliziaji

Amesema kwa sasa maisha ni nyumba hivyo wananchi wakijitokeza kununua nyumba hizo kutasaidia serikali kupata fedha ambazo zitawezesha nyumba nyingine kujengwa katika maeneo mbalimbali ya nchi ili huduma hiyo iwafikie wananchi wengi wenye lengo la kuwa na makazi bora

Awali akizungumza mbele ya naibu waziri mhandisi wa ujenzi kutoka shirika la Nyumba la Taifa NHC Bw Edward John ameelezea hatua za ujenzi huo kwa kusema kuwa nyumba 30 zipo katika hatua za mwisho za umaliziaji wa ujenzi wake ambapo zinatarajiwa kumalizika hivi karibuni


Naye meneja mauzo wa NHC Bw. Erasto Chilambo amesema tayari wameshafanya matangazo ya kutosha kuhusu ununuzi wa nyumba hizo, na gharama za kuuza nyumba moja ni Zaidi ya shilingi milioni 54 za kitanzania pamoja na VAT na shilingi milioni 46 bila VAT

Sikiliza sauti hapa chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo