Aibu: Baba Amgeuza Binti Yake Mlemavu Kuwa Mkewe, Sikiliza Sauti hapa

Serikali wilayani Chunya mkoani Mbeya inamshikilia mwanaume mmoja aitwaye Maneno Pesambili Kanjanja (59) akituhumiwa kumuingilia kimwili binti yake wa kumzaa na kumfanya kama mkewe katika kitongoji cha Mwakambonja kijiji cha Kiwanja Kata ya Mbugani

Tukio hilo la kikatili limetokea Januari 22 mwaka huu Majira ya saa mbili usiku baada ya binti huyo ambaye ni mlemavu kuokotwa na wasamaria wema akiwa anakwenda kujihifadhi kwenye jengo la CCM lililopo mita 100 kutoka nyumbani kwao huku akitambaa

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mh Rehema Madusa amefika eneo la tukio na kuzungumza na wananchi waliofurika eneo hilo na kuviagiza vyombo vya ulinzi na usalama hasa jeshi la polisi kuhakikisha wanasimamia suala hilo katika vyombo vya sheria ili haki itendekea 

Msikilize Mkuu wa wilaya akizungumzia tukio hilo:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo