Picha: Mvua zakwamisha Usafiri Songwe, Mabasi yakwama

MAGARI ya abiria yanayofanya safari zake kati ya Kamsamba na Mlowo mkoani Songwe jana yalikumbwa na wakati mgumu kiasi cha kusitisha safari zake kwa muda kutokana na maji ya mitaro yaliyotokana na mvua kubwa sambamba na utelezi kuhatarisha usalama wake na abiria.


Kwa ujumla barabara ya Kamsamba hadi Mlowo ambayo ni ya changarawe, imeendelea kuathiriwa na maji yanahoporomoka kwa kasi na kuondoa vipande vya barabara pembezoni hivyo kupunguza upana wake. 

Pichani moja ya mabasi yanayofanya safari eneo hilo lilisimama kwa takriban saa 2 kusuburi maji yapungue ndipo liendelee na safari baada ya mkondo wa maji ya mvua kumega sehemu ya barabara na hivyo kuhatarisha usalama wa magari yanayopita eneo hilo
Chanzo:Mbeya yetu blog


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo