Wazika maiti si yao, wafukua na kuzika upya

Ukistaajabu ya Musa, utayaona ya firauni. Hivyo ndivyo unavyoweza kusema baada ya ndugu wa familia ya marehemu Gudluck Munuo (53), mkazi wa Kijiji cha Mese, Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro, kuchukua maiti ya mtu mwingine iliyokuwa imehifadhiwa katika Hospitali ya Kibong'oto na kwenda kuzika.


Tukio hilo limezua taharuki, lilitokea Mei 26, mwaka huu wakati ndugu hao bila kujua, walichukua maiti ya Eliudi Mbaga (68) ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Matadi.

Hata hivyo, ndugu wa marehemu Mmbaga walipoenda kuchukua mwili katika hospitali hiyo ya Kibong'oto walikuta mwili wa ndugu yao haupo ndipo walipofuatilia kwa kushirikiana na uongozi wa hospitali hiyo na kubaini umeenda kuzikwa katika Kijiji cha Mese.

Baada ya kufanya taratibu zinazotakiwa Mei 26, mwili huo ulifukuliwa na kukabidhiwa kwa ndugu wa marehemu Mbaga na ulizikwa siku hiyo hiyo. Mwananchi lilifanikiwa kuzungumza na Mkuu wa Wilaya hiyo, Dk Christopher Timbuka alikiri kuwapo kwa tukio hilo na ndugu wameshachukua miili ya ndugu zao na kwenda kuizika.” alisema

Akisimulia mkasa huo, mmoja wa wakazi wa Kijiji cha Mese, Alex Munuo alisema changamoto iliyojitokeza ni kwa waliopeleka maiti hospitali si waliokwenda.

"Hili tukio kweli limezua taharuki kidogo hapa kijijini maana ni tukio la kushangaza, mimi ndiye niliyepeleka mwili wa Gudluck Munuo hospitali lakini siku ya kwenda kuchukua mwili sikwenda mimi walienda ndugu wengine," alisema.

“Muda ambao tunaaga mwili wa marehemu baada ya kufikishwa hapa nyumbani kwake tuliingiwa na wasiwasi kidogo kama vile mwili ulikuwa umebadilika, tukajiuliza mbona kama sio yeye, tuliitana pembeni lakini tuliona labda kwa kuwa mwili ulikuwa mochwari ulibadilika rangi, hivyo tuliamua kuzika, lakini baadaye ndio ikaja kubainika si yeye, tukalazimika kufukua Mei 26 na kuukabidhi kwa wahusika na sisi tukachukua mwili wetu tukazika siku ileile."

Akisumulia namna walivyoenda kuchukua mwili hospitalini na kuukosa, ndugu wa familia ya Mmbaga, Kiloliki Mbaga alisema walipofika hospitali mwili wa ndugu yao wahudumu waliwaongozana kwenda chumba cha maiti na walishangaa walipofungua sanduku walikuta maiti siyo yao.

Naye, Mwenyekiti wa Kijiji cha Matadi wilayani humo, Asanterabi Ng'unda alitaka umakini uwepo kwa wanaokwenda mochwari kuchukua miili ya wapendwa wao


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo