AUDIO: Mkuu wa wilaya ya Ludewa Azungumzia Ishu ya Ushirikina

Mkuu wa wilaya ya Ludewa mkoani Njombe Mh Patrick Tsere amekemea tabia ya ushirikina inayoelekezwa kwa baadhi ya walimu wilayani mwake kwani inachangia kurudisha nyuma maendeleo ya elimu

Mkuu huyo wa Wilaya ametoa kauli hiyo wakati akitoa mchango wake kuhusu sekta ya elimu katika kikao cha kamati ya ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika leo mkoani Njombe, ambapo amesema pamoja na jitihada zinazofanywa na serikali kuboresha elimu bado wapo wanajamii wanaowatisha walimu na wengine kudiriki kuwafanyia vitendo vya kishirikina vinavyosababisha walimu kukimbia ama kuondoka na kuacha kufanya kazi hiyo

Amesema wakishaondoka inapelekea wilaya na mkoa kwa ujumla kuwa na upungufu mkubwa wa walimu ili hali jambo hilo halitakiwi kufanywa na wanajamii badala yake washirikiane na walimu kuleta maendeleo ya elimu kwa manufaa ya watoto wao na taifa kwa ujumla

Pia mkuu huyo wa wilaya ameshangazwa na baadhi ya wabunge wa mkoa wa njombe kulalamika katika kikao hicho kuhusu kuchelewa kwa pembejeo za kilimo, na kusema hawatakiwi kushangaa kwa kuwa wao ndio walipitisha bajeti ya wizara hiyo na kwa nini hawakushikilia shilingi ya bajeti hiyo

Amesema malalamiko yao katika kikao hicho hayasaidii badala yake waongee na waziri wa kilimo moja kwa moja kumweleza changamoto za wilaya zote za mkoa wa Njombe kuhusiana na kilimo kwa kuwa kila wilaya ina changamoto zake, hivyo pembejeo kuchelewa bado linaendelea kujitokeza licha ya maazimio ya vikao mbalimbali kuazimia pembejeo zisicheleweshwe

Sikiliza sauti zake hapa chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo