Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Nchini -TAA imesema watu waliojimilikisha na kupima viwanja katika Uwanja wa Ndege wa Mbeya hawakuishirikisha wala kuruhusiwa na Mamlaka hiyo.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa TAA, Lawrent Mwigune amemweleza mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makala kuwa uuzwaji wa viwanja ndani ya uwanja wa ndege wa Mbeya, unafanyika kimakosa.
Kufuatia hali hiyo Mkuu wa mkoa wa Mbeya ameuagiza uongozi wa mamlaka ya viwanja vya ndege nchini kukutana na watu waliouziwa viwanja vya makazi ndani ya uwanja huo wa ndege wa Mbeya na kutoa maelezo kamili juu ya viwanja vilivyopimwa kwa ajili ya makazi.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa TAA, Lawrent Mwigune amemweleza mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makala kuwa uuzwaji wa viwanja ndani ya uwanja wa ndege wa Mbeya, unafanyika kimakosa.
Kufuatia hali hiyo Mkuu wa mkoa wa Mbeya ameuagiza uongozi wa mamlaka ya viwanja vya ndege nchini kukutana na watu waliouziwa viwanja vya makazi ndani ya uwanja huo wa ndege wa Mbeya na kutoa maelezo kamili juu ya viwanja vilivyopimwa kwa ajili ya makazi.