Jeshi la polisi mkoani Shinyanga linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kuchoma ofisi ya mwalimu mkuu shule ya msingi Ibanilo iliyoko katika kijiji cha Igembya kaya ya Nyida wilayani Shinyanga.
Kwa mujibu wa kituo cha ITV ambacho kimefika katika shule hiyo na kukuta wakazi wa maeneo hayo wakiwa katika hali ya taharuki huku wakidai kuwa kumekuwepo na mgogoro wa ardhi unaufukuta muda mrefu kati wakazi wawili ambao majina yao yamehifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi na uongozi wa shule hali ambayo imekuwa ikisababisha vitisho vya mara kwa mara na uharibifu wa mali za shule.
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Ibanilo Bw.Shabani Jumanne ameainisha hasara iliyotokana na kuchomwa kwa ofisi hiyo na kuomba msaada wa haraka kwa wadau wa elimu kabla shule hazijafunguliwa mwezi January Mwakani huku diwani wa kata ya nyida Mh.Selemani Segeleti sakikiri kiwepo kwa mgogoro wa muda mrefu ambao amekua akiushughulikia bila mafanikio.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa jeshi mla polisi mkoani Shinyanga ACP Muliro Jimanne Muliro amesema licha ya kuwakamata watu hao wawili kwa tuhuma za kuhusika kuchoma na kuharibu mali ya umma jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi zaidi ili na hatua za kisheria zitachukuliwa ikiwemo watuhumiwa kufikishwa mahakamani.