Chama cha kutetea Abiria Chapigwa Marufuku na Kamanda Mpinga

Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani nchini DCP Mohamed Mpinga amesitisha utendaji wa chama cha Kutetea Abiria Taifa (CHAKUA) kuendelea na shuguli zake katika mikoa yote nchini isipokuwa kwa mkoa wa Dar es Salaam pekee

Akitaja sababu za kusitisha utendaji wa chama hicho jana  jijini Dar es Salaam wakati akitoa ripoti ya namna walivyojipanga kuzuia ajali za Barabarani DCP Mpinga alisema, utendaji mbaya na kukiuka maadili na kujikita katika usimamizi wa sheria badala ya kutoa elimu unaofanywa na chama hicho ndiyo sababu ya kusitishwa kwa utendaji wao na kwamba kuanzia sasa shughuli zao zitafanywa na Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Muda mfupi baada ya kutolewa kwa tamko hilo, Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Kutetea Abiria Taifa, Bwana Hassan Mchanjama alikanusha tuhuma hizo huku akisema kuwa, kuzuia utendaji wa chama cha abiria kwa kile alichokiita ni maslahi binafsi ni kuwanyima wananchi mahala pa kuwasilisha kero zao ambapo amebainisha kuwa chama hicho hakijawahi kukiuka taratibu zake za utendaji kama ilivyoelezwa.

Mbali na suala hilo DCP Mohamed Mpinga amewataka wamiliki wa magari kote nchini kuondoa na kuacha mara moja kutumia taa zenye mwanga mkali maarufu kwa jina la 'Sportlights' katika vyombo vyao vya moto kwani taa hizo ziimekuwa kero kwa madereva wengine na kuchangia ajali za barabarani nchini.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo