Wafungwa wakosa sare, Walazimika kukaa Uchi Gerezani mkoani Katavi

Imebainika kuwa wafungwa wa Gereza la Kalilankulukulu lililopo wilayani Tanganyika mkoani Katavi licha ya kukosa sare za wafungwa Gerezani na kuwasababishia kukaa Utupu, wafungwa hao pia wanakabiliwa na ukosefu wa maji safi na salama

Hali hiyo inawasababishia pia kutembea kwa miguu kwa umbali mrefu wa kilometa 10 kuyatafuta maji

Hayo yamesemwa na mkuu wa gereza hilo Samwel Obete Lulu wakati akitoa taarifa kwa mbunge wa viti maalum Mkoani Katavi Tasika Mbugo pindi alipotembelea gereza hilo kwa ajili ya kuzungumza na wafungwa

Mbali na changamoto hiyo wafungwa hao hulazimika kulia chakula mikononi badala ya vyombo maalum

Mbunge huyo amejitoa kwa kuwakabidhi shilingi 336,000/= kwa ajili ya kununua vikombe, bakuli na sabuni za kuogea



Mkuu wa wilaya hiyo Salehe Mhando amemshukuru mbunge huyo kwa moyo wake wa kujitolea huku akiiomba wizara ya mambo ya ndani ya nchi kuliangalia suala la wafungwa wa gereza hilo na kulitatua kwani linakiuka haki za binadamu


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo