Mwanafunzi wa shule ya Msingi Rufita iliyoko mkoani Tabora mwenye umri wa
miaka 13 ameozeshwa kinyemela na mama yake Mzazi na kukatishwa masomo
Mwanafunzi huyo anayeishi na mwanaume anayejulikana kwa jina la Bakari
Abdul Kwa muda wa miezi mitatu sasa huku mzazi wa mwanafunzi huyo akidai hajui
mwanaye aliko
Walimu wa mwanafunzi huyo ambaye jina lake limehifadhiwa wamesema alikuwa
mtoro na kwamba mzazi wake hakuwa akitoa ushirikiano kwao
Afisa mtendaji wa kata ya Mbugani ilipo shule hiyo Imakulata Gembe amesema
wamechukua hatua ikiwemo kuwakamata wazazi wa mwanafunzi huyo ili iwe fundisho
kwa wengine
Hivi karibuni Mkuu wa mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri aliagiza mkuu wa wilaya
kuwashughulikia wale wote wanaowakataza watoto wa kike wasisome na kwamba wawe
wakali hata kwa wazazi
