wahitimu hao
Wahitimu wa Kidato cha Nne wilayani Makete mkoani Njombe
wametakiwa kutii mamlaka zilizopo katika maeneo yao watakayokwenda baada ya
kuhitimu masomo yao
Hayo yamesema jana na Mgeni Rasmi Mh Sarah Shembekeza
katika mahafali ya 22 ya kidato cha Nne katika shule ya Sekondari Mwakavuta,
ambapo amewasisitiza wanafunzi hao kuwa mbali na kuhakikisha wanafanya vema
katika mtihani wa kuhitimu kidato cha nne lakini pia watambue kuna mamlaka
watakazokutana nazo baada ya kuhitimu na wanatakiwa kuziheshimu
Pia amewaonya suala la kuvaa mavazi isivyokubalika
Amewataka wawapo vijijini kujiepusha na makundi mabaya
yatakayoweza kuwashawishi kujiingiza kwenye matumizi ya dawa za kulevya na
utumiaji wa pombe
Akijibu baadhi ya changamoto Mh Shembekeza amesema
atapigania kuhakikisha kero ya maji inayoikabili shule hiyo kutokana na
ongezeko la watumiaji wa huduma hiyo linamalizika kutokana na mipango ambayo
imewekwa na halmashauri ya wilaya ya Makete
Katika mahafali hayo Mkuu wa shule hiyo Mwalimu Lukas
Mkakatu akazungumzia pia baadhi ya mafanikio ya shule hiyo
Nao wahitimu hao wamezungumzia matarajio yao ikiwemo pia
kufanya vizuri katika mtihani wao wa kuhitimu kidato cha nne unaotarajiwa
kuanza Novemba Mosi Mwaka huu



