Mwamuzi aibiwa simu akichezesha mechi CCM Kirumba Mwanza

Ni aibu ya aina yake katika soka la bongo. Pale mwamuzi wa akiba wa mchezo kati ya Toto African dhidi ya Mbeya City Joseph Masija alipoibiwa simu mbili za mkononi zenye thamani ya shilingi 500,000 na fedha taslim 140,000. 

Vitu hivyo viliibwa kwenye vyumba vya waamuzi hapo CCM Kirumba. Ni jambo la kuaibisha kama nini? Swali linalokuja kichwani kwangu ni hili: 

Uongozi wa uwanja huo umeshindwa kuweka ulinzi wa kutosha kwenye vyumba vilivyopo hapo uwanjani?? Swala la usalama wa watu na mali yao ni jambo ambalo ni lazima lipewe kipaumbele. Ina maana hata usalama wa waamuzi wenyewe uko mashakani. 

Kama anaweza kuingia vyumba vya waamuzi bila mtu yoyote kumuona na kuiba vitu, Je hawezi akamuwekea mwamuzi vitu vyenye kuhatarisha uhai. Tafadhali hili jambo liangaliwe kwa jicho la kipekee ili lisijirudie tena

chanzo: michezoforums


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo