CHADEMA watuma salamu Kwa Jeshi la Polisi kuwa waamue "kusuka au Kunyoa"

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),kimelitaka jeshi la polisi kuwaachia au kuwapeleka mahakamani watu 10 wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa chama hicho.

Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu amewaambia wanahabari leo kuwa watu hao walikamatwa katika mikoa mbalimbali ukiwamo wa Songwe kwa kosa la kuandika na kusambaza maneno yasiyomfaa Rais John Magufuli.

Lissu amesema watu wapo mahabusu za Polisi Kanda Maalumu na Osterbay takriban wiki zaidi ya mbili jambo ambao ni kinyume cha sheria za nchi na kwamba wanapewa mateso.

"Nimekwenda kuonana nao na wamenieleza madhara wanayoyapata kutoka kwa polisi,"amesema Lissu.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo