Waumini waingia kanisani na Mabango ya Kumpinga Askofu

Waumimi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Dayosisi ya Kusini Mashariki, Kanisa Kuu la Mtwara wameingia katika ibada na mabango yaliyokuwa na ujumbe mbalimbali wa kumpinga Askofu Mkuu wa dayosisi hiyo, Lucas Mbedule kwa tuhuma za kukiuka katiba, unyanyasaji wa watumishi na ubadhilifu wa fedha za ushirika na dayosisi. 

Hata hivyo, Askofu Mbedule amesema asingependa kuyazungumzia suala hilo kwa sababu walikaa kikao. 

Umoja wa wazee ulitoa tamko ndani ya kanisa hilo kutokana na tuhuma zinazomkabili askofu huyo na kumtaka asijihusishe na mambo yanayohusu usharika na dayosisi, ili kupisha uchunguzi na kumwomba Mkuu wa KKKT, Dk Fredrick Shoo kuunda tume kuchunguza tuhuma hizo. 

Akisoma tamko la wazee wa kanisa hilo, Amon Mkocha amesema wanapinga uamuzi uliofanywa na kikao cha halmashauri kuu kilichofanyika mwezi huu


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo