Msemaji wa CCM ampongeza Lowassa

Msemaji wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Christopher Ole Sendeka amesema Edward Lowassa ni muungwana na kwamba asingeweza kuacha kumsalimia kwa kumpa mkono Rais John Magufuli. Ole Sendeka amesema jana: 

“Namfahamu Lowassa ni muungwana hawezi kuacha kusalimiana kwa kupeana mkono na Rais. Wamekutana viongozi, Rais na waziri mkuu mstaafu hawawezi kuacha kusalimiana.” 

Lowassa ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema aliyechuana na Rais Magufuli katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015 mwaka jana, juzi walikutana kwa mara ya kwanza na mpinzani wake huyo tangu kinyang’anyiro hicho kilipomalizika. 

Viongozi hao walikutana kwenye misa ya jubilei ya dhahabu ya ndoa ya Rais mstaafu, Benjamin Mkapa na mkewe Anna katika Kanisa la Mtakatifu Petro.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo