Washikiliwa na polisi kwa ukatili wa kijinsia


Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma Lazaro Mambosasa.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linawashikilia watu sita kwa makosa mbalimbali yanayohusu ukatili na unyanyasaji wa kijinsia.

Katika kipindi kifupi kumekuwa na matukio ya aina hiyo ambayo pia mengine yamesababisha mauaji ambayo chanzo chake ni mahusiano ya kimapenzi na ulevi kupindukia.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkoani Dodoma, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma Lazaro Mambosasa amesema vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia ni kosa kisheria, lakini watu wamekuwa wakivinyamazia vitendo hivyo kwa kuwa vinahusisha watu wa karibu baina ya watendewa na wahalifu.

Uhalifu huo unawaathiri zaidi watoto wadogo ambapo yapo matukio ya kujeruhi watoto, kuua na kutupa watoto ambapo Kamanda Mambosasa ametumia fursa hiyo kuwataka wananchi wa Dodoma kutokaa kimya dhidi ya wahalifu wa aina hiyo

Kamanda Mambosasa amewataka wananchi watoe taarifa katika vituo vya polisi na watumie vema madawati ya jinsia na watoto yaliyopo katika vituo vya polisi vya wilaya zote za Dodoma.

Watuhumiwa waliokamatwa watafikishwa mahakamani mara upelelezi utakapo kamilika.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo