Mkuu wa wilaya ya Iringa awashikisha adabu Walinzi wa Hospitali ya Rufaa ya Iringa

Maneno kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya Iringa "jana saa 3 na dakika 25 Usiku nilipokea wakina mama 3 wakiwa wanatetemeka kwa baridi, wakilalamika kumwagiwa maji walipokuwa wamekaa kwenye eneo la kusubiria wagonjwa walio lazwa hasa kwa wale walio toka mbali. 

Maji hayo yalimwagwa na walinzi wa kampuni ya Amazon ambao ndio wamepewa kandarasi ya ulinzi hospitali ya Rufaa ya Iringa. 

Nilifika hospitali kujionea mwenyewe hali halisi, baadae nikapata taarifa kuwa jana yake Mlinzi alimpiga mzee aliyekuwa ameleta chakula hospitali na kumwaga kwa mateke. 

Niliamuru mlinzi huyo na mwenzake wakamatwe pia mwenye kampuni afike kituo cha polisi haraka iwezekanavyo. 

Hali hii imeudhi sana hasa ukiona jinsi wakina mama walivyo nyanyasika wengine vyombo vyao na chakula kuroweshwa maji."


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo