Mke wa bilionea Msuya kortini Kwa Mauaji ya Aneth Msuya


MKE wa bilionea Erasto Msuya, Miriam Elisaria Msuya (41) amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya dada wa wa bilionea huyo, Aneth Msuya.

Mshtakiwa huyo alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana jijini Dar es Salaam na kusomewa mashtaka na Wakili wa Serikali, Diana Lukondo mbele ya Hakimu Mkazi, Margareth Bankika.

Akisoma mashtaka hayo, Lukondo alidai mshtakiwa huyo ambaye ni mkazi wa maeneo ya Sakina kwa Iddi, jijini Arusha anadaiwa Mei 25, mwaka huu katika maeneo ya Kibada Kigamboni jijini Dar es Salaam alimuua Aneth Elisaria Msuya.

Mshtakiwa hakutakiwa kujibu lolote kwa sababu mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi za mauaji, mbapo Jamhuri ilidai upelelezi haujakamilika na kuomba kesi hiyo ipangwe tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Hakimu Bankika, alikubali kuahirisha kesi hiyo hadi Septemba 9, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa na mshtakiwa alirudishwa rumande.

Habari zilizopatikana baada ya tukio hilo zilidai kwamba, marehemu Aneth aliuawa kwa kuchinjwa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia Mei 25, mwaka huu Dar es Salaam. 

Mauaji hayo yalitokea nyumbani kwake eneo la Kibada block 16, Kigamboni ambako inaelezwa wauaji hao hawakuchukua kitu chochote ndani ya nyumba yake.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo