Na Fadhili Lunati
Baadhi ya wakulima katika kata ya Tandala wilayani Makete mkoani Njombe wamelalamikia kitendo cha Afisa kilimo kutowafikia wakulima ipasavyo katika maeneo yao jambo ambalo wamedai limekuwa likichangia kwa kiasi kikubwa wakulima hao kupata mavuno hafifu.
Wakizungumzia changamoto hiyo wakulima hao wamesema hali hiyo imekuwa ikiwakosesha haki yao ya msingi ya kupata elimu ihusuyo kilimo kwani Maafisa kilimo waliletwa kwa ajili ya kuwasaidia wakulima.
Aidha wakulima hao wamesema kuwa wakati mwingine changamoto inayochangia maafisa kilimo kutowafikia wakulima ipasavyo ni kukaimu shughuli nyingine za kiutawala, hivyo wameitaka serikali kuitatua changamoto hiyo kwani imekuwa ikiathiri shughuli za kiutendaji.
Akijibu malalamiko hayo Afisa kilimo kijiji cha Tandala ambaye pia ni Kaimu Afisa Kilimo kata ya Tandala Bw. Bruno Mhiche amesema si kweli kwamba yeye hawafikii wakulima bali wakulima wamekuwa ni waoga kumtumia na kuongeza kuwa utaratibu unahitaji mkulima afike katika ofisi ya kijiji kukutana naye ili aweze kumsaidia.
Kuhusu kukaimishwa majukumu ya kiutawala Bw.Mhiche amesema si kweli kwamba limekuwa likiathiri utendaji kama inavyoelezwa na baadhi ya wakulima isipokuwa hali hiyo hutokea pale inapotokea dharura kwa viongozi husika.
Pia Bw.Mhiche ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa wakulima kuwatumia wataalamu wa kilimo walio kwenye maeneo yao ili waweze kuondokana na kilimo cha mazoea na kuendana na kilimo cha kisasa chenye tija kwa mkulima.
Wakizungumzia changamoto hiyo wakulima hao wamesema hali hiyo imekuwa ikiwakosesha haki yao ya msingi ya kupata elimu ihusuyo kilimo kwani Maafisa kilimo waliletwa kwa ajili ya kuwasaidia wakulima.
Aidha wakulima hao wamesema kuwa wakati mwingine changamoto inayochangia maafisa kilimo kutowafikia wakulima ipasavyo ni kukaimu shughuli nyingine za kiutawala, hivyo wameitaka serikali kuitatua changamoto hiyo kwani imekuwa ikiathiri shughuli za kiutendaji.
Akijibu malalamiko hayo Afisa kilimo kijiji cha Tandala ambaye pia ni Kaimu Afisa Kilimo kata ya Tandala Bw. Bruno Mhiche amesema si kweli kwamba yeye hawafikii wakulima bali wakulima wamekuwa ni waoga kumtumia na kuongeza kuwa utaratibu unahitaji mkulima afike katika ofisi ya kijiji kukutana naye ili aweze kumsaidia.
Kuhusu kukaimishwa majukumu ya kiutawala Bw.Mhiche amesema si kweli kwamba limekuwa likiathiri utendaji kama inavyoelezwa na baadhi ya wakulima isipokuwa hali hiyo hutokea pale inapotokea dharura kwa viongozi husika.
Pia Bw.Mhiche ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa wakulima kuwatumia wataalamu wa kilimo walio kwenye maeneo yao ili waweze kuondokana na kilimo cha mazoea na kuendana na kilimo cha kisasa chenye tija kwa mkulima.
Sikiliza sauti hii:-
