Njombe Kidedea kwa Usafi nchi Nzima, yajishindia Gari

Halmashauri ya wilaya ya Njombe Mkoani Njombe imetangazwa mshindi wa jumla kwenye usafi wa mazingira nchini na kukabidhiwa Gari baada ya takwimu kuonesha halmashauri hiyo kutokuwa na mgonjwa hata mmoja aliyekumbwa na ugonjwa wa kipindupindu

Kwa mujibu wa wizara ya afya ushindi huu unaashiria kwamba Njombe imefanya vizuri zaidi mbele ya majiji manispaa na halmashauri nyinginezo nchini

Valentino Hongoli ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Njombe ameeleza mikakati iliyofanikisha wao kuibuka kidedea kuwa ni pamoja na wataalamu wake kupita vijijini kuelimisha wananchi juu ya utunzaji wa mazingira

Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Ummi Mwalimu ameelezea vigezo vilivyoangaziwa katika ushindani huo ambapo miongoni mwa vigezo hivyo ni matumizi ya vyoo bora

Sikiliza Sauti hii


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo